Home
Dar Leo
Makomandoo wa Kikosi Maalumu cha Majini cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
Thursday, 02 September 2010 12:47

Makomandoo wa Kikosi Maalumu cha Majini cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakifanya onesho la uokoaji wa mateka kwenye 'Kisiwa' jana ikiwa ni sehemu ya ufungaji wa maadhimisho ya miaka 46 ya jeshi hilo. (Picha na Charles Lucas)

 
Moto wateketeza makaburi
Thursday, 02 September 2010 12:39



Na Waandishi Wetu, jijini/Morogoro

UMATI wa ndugu uliojaa simanzi ulifurika jana katika makaburi ya Kola, mjini Morogoro baada ya moto kuzuka ghafla na kuteketeza zaidi ya makaburi 100.

Baadhi ya ndugu walifika eneo hilo walijikuta wakiangua vilio baada ya kushuhudia moto huo ukiendelea kushika kasi katika makaburi hayo ya Wakristo huku ukiteketeza misalaba yote na uharibifu mwingine katika makaburi hayo.

 
Makamba amcharukia Shibuda
Thursday, 02 September 2010 12:30



Na Dunstan Bahai,Jijini

KATIKA hali inayoonesha joto la kampeni za uchaguzi linazidi kupanda, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, amemjia juu mgombea Ubunge wa Jimbo la Maswa Magharibi kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Shibuda, na kumfananisha na ‘mwenda wazimu’.

 
Maisha ya Watanzania mashakani
Thursday, 02 September 2010 12:35



Na Christina Gauluhanga, jijini

WANANCHI wameingiwa na hofu kuhusu afya zao baada ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kutangaza rasmi kuruhusu matumizi ya dawa ya Meltakelfin kutoka Italia ambayo ilipigwa marufuku kwa madai kuwa hazikukidhi viwango vya ubora uliotakiwa.

 
CHADEMA yazidi kumkalia kooni JK
Tuesday, 31 August 2010 11:23

Na Grace Ndossa, jijini

MSAJILI wa Vyama vya Siasa Nchini, John Tendwa, amesema amepokea pingamizi la malalamiko ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) dhidi ya mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo asubuhi, Tendwa amesema uamuzi wa pingamizi hilo juu ya Sheria za Gharama za Uchaguzi utatolewa baada ya siku tano ambapo ataita pande zote mbili ili ziweze kutoa maelezo ya kina.

Ameongeza kuwa baada ya kusikiliza pande zote atawasilisha nakala kwa Mkurugenzi wa Uchaguzi pamoja na makatibu wakuu wa vyama vyote viwili.

Amesema sheria ya gharama za uchaguzi ni tofauti na Ilani ya Chama, hivyo baada ya uamuzi huo ambaye hataridhika ana haki ya kwenda kwenye chombo cha sheria kwa ajili ya kutafuta haki zaidi.

CHADEMA iliazimia kumwekea pingamizi mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa madai kuwa amekiuka sheria ya gharama za uchaguzi kwa kutangaza nyongeza ya mishahara kwenye kampeni na hivyo azuiwe kugombea urais.

 

 
<< Start < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > End >>

Page 1 of 47

Swali la Leo

Website is used for?
 

Walio Kwenye Mtandao

We have 12 guests online
mod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_countermod_vvisit_counter
mod_vvisit_counterToday334
mod_vvisit_counterYesterday871
mod_vvisit_counterThis week4226
mod_vvisit_counterLast week4920
mod_vvisit_counterThis month1987
mod_vvisit_counterLast month22527
mod_vvisit_counterAll days50607

We have: 10 guests, 2 bots online
Your IP: 38.107.191.106
 , 
Today: Sep 03, 2010