ZAIDI ya wakazi 300 wa Kipawa waliobomolewa nyumba zao licha ya kugoma kupokea fidia zao leo asubuhi wamevamia katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi huku wakilia na kuazimia kuishtaki Serikali kutokana na kubolewa makaburi yao ambayo hayajafidiwa bado.
MOTO mkubwa umezuka katika ghorofa la Sophia House lililopo katika makutano ya Mtaa wa Bibi Titi na Azikiwe na kusababisha tafrani kwa wafanyakazi waliokuwemo ndani na wapita njia.
MOTO mkubwa umezuka katika ghorofa la Sophia House lililopo katika makutano ya Mtaa wa Bibi Titi na Azikiwe na kusababisha tafrani kwa wafanyakazi waliokuwemo ndani na wapita njia.
Tukio hilo limetokea leo asubuhi saa moja ambapo chanzo chake bado hakijafahamika.
Mwandishi wa gazeti hili alishuhudia baadhi ya wafanyakazi wakihaha huku na kule ili kuokoa maisha yao ambapo hata hivyo wangene walinusurika kugongwa na magari yaliyokuwa yakipita kasi katika eneo hilo.
Inadaiwa kuwa moto huo ulianzia kwenye ofisi za Shirika la Ndege la South Africa ambapo haikuweza kufahamika mara moja umesababishwa na nini.
Gazeti hili lilishuhudia gari la Kikosi cha Zimamoto cha Jiji STK 4372 likiwahi kufika eneo hilo na kuzima moto huo ili usilete madhara zaidi katika jengo hilo.
Hata hivyo gazeti hili lilimtafuta msemaji wa ofisi hizo lakini jitihada zilikwama kwa madai kuwa alikuwa bado hajafika.Chanzo na thamani ya mali iliyotekea bado haijafahamika.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile hakuweza kupatika kwa njia ya simu kuzungumzia tukio hilo kwakuwa simu yake ya mkononi ilikuwa ikiita bila kupokelewa.
Dhamana yasababishwa kesi ya DECI ipigwe kalenda
Monday, 08 February 2010 12:04
Na Waandishi Wetu, Kisutu
KESI inayowakabili vigogo wanne wa kampuni ya upatu ya Development Enterpreneurship Community Initiative (DECI), imeshindwa kuendelea kuunguruma leo kutokana na jalada limepelekwa Mahakama Kuu kwa ajili ya maombi ya dhamana.
VIKOSI vya uokozi nchini Lebanon vimefanikiwa kupata kisanduku cheusi kilichokuwa kikitumika kutunza kumbukumbu katika ndege ya Shirika la ndege la Ethiopia iliyoanguka katika mwambao wa bahari ya Mediterranian hivi karibuni
WATU watano wameripotiwa kufa na wengine 12 wamejeruhiwa baada ya kutokea mlipuko katika kituo cha kuzalisha umeme kinachoendeshwa kwa gesi katika jimbo la Connecticut nchini Marekani.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani nchini Uingereza, Alan Johnson, amesema kuwa serikali itapunguza idadi ya visa kwa wanafunzi wa kigeni ili kukomesha matumizi mabaya ya mfumo huo.