|
Mwanafunzi afa maji akienda kusalimia |
|
Monday, 30 August 2010 13:02 |
|
Na Christina Gauluhanga, Polisi
OMARY Mohamed (9), mwanafunzi wa darasa la tatu kutoka Shule ya Msingi Tandika Azimio, mkazi wa Tandika, amekufa baada ya kuzama maji wakati akiogolea mto Kizinga, Kivule wilaya ya Ilala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Missime, amesema tukio hilo limetokea jana saa 7 mchana Mto Mzinga.
Imedaiwa kuwa mwanafunzi huyo na mama yake, Amina Omary (30), mkazi wa Tandika, walikwenda Kivule kusalimia ndugu zao ambapo mtoto huyo alitoka na kwenda kuogelea na wenzake.
|
|
|
Mgombea aahidi kuineemesha Ukonga |
|
Monday, 30 August 2010 13:01 |
|
Stella Aron na Christina Gauluhanga, Ukonga
MGOMBEA ubunge Jimbo la Ukonga kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Eugen Mwaiposa, amewaasa wananchi wa jimbo hilo kukipigia kura chama hicho ili kuweza kubadilisha sura ya jimbo hilo na kuleta maendeleo ya haraka.
Akizungumza na gazeti hili, mgombea huyo amejigamba kuwa endapo atachaguliwa kuingia atahakikisha kuwa wananchi wa jimbo hilo wanapata maji ya bomba.
|
|
Mchinga kizimbani akidaiwa kuiba magari |
|
Monday, 30 August 2010 12:58 |
|
Na Halima Kilagu, Temeke
MSHITAKIWA Yahya Mchinga (26), mkazi wa Kurasini, amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temake kujibu mashitaka ya wizi wa gari.
Mshitakiwa amesomewa mashitaka na Mwendesha Mashitaka Issaya Mwanga mbele ya Hakimu Rose Kagwa.
Imedaiwa mahakamani hapo kuwa Agosti 2, mwaka huu, saa 6 usiku, mshitakiwa aliiba gari mbili aina ya Isuzu zenye thamani ya sh. 50,000,000, mali ya Adolf Emmanuel.
|
|
|
Wanafunzi waanguka mashetani |
|
Monday, 30 August 2010 13:00 |
|
Na Khadija Idd, Tabata
VILIO na simanzi vimetawala leo katika Shule ya Msingi Tumani ambako zaidi ya wanafunzi 26 wameanguka ghafla na kuanza kupiga mayowe wakidai wanawaona watu walio uchi wa mnyama.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu tukio hilo limetokea leo saa 2 asubuhi ambapo wazazi na walezi walilazimika kutinga katika shule hiyo kwa ajili ya kuokoa maisha ya watoto wao.
Hali hiyo imezua tafrani kati ya wazazi na walimu hao ambapo kwa msaada wa haraka walikuwa wakiwachukua watoto wanaodondoka kisha kuwakimbiza kwenye kanisa la Assembles Of God lililopo jirani kwa ajili ya kuombewa.
|
|
Kimanga waomba barabara zifanyie ukarabati |
|
Monday, 30 August 2010 12:51 |
|
Na Shaaban Mkumbwa, Tabata
WAKAZI wa Kimanga Darajani wameiomba Manispaa ya Ilala kwa kushirikiana na Serikali ya Mtaa kukarabati barabara ambazo zimekuwa kero kwa kipindi kirefu kutokana na kushindwa kupitika.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, wakazi hao wamedai kuwa barabara hizo ziliharibiwa na mvua na kusababisha kuwapo kwa madimbwi yanayosababisha kero wa madereva na kusababisha kuwepo kwa kero ya usafiri.
Wamedai kuwa kutokana na kuwepo kwa mashimo hayo hivi sasa katika barabara itokayo kituo cha Savana kuelekea Tabata AMI haipitiki kutokana na kuwapo kwa mashimo makubwa.
|
|
|
|
|
<< Start < Prev 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 Next > End >>
|
|
Page 3 of 47 |